Header ads

Header ads
» » Malipo ya deni la Zantel kuelekezwa katika ujenzi wa madarasa 40 Kinondoni



KAMPUNI ya simu za mkononi ya Zantel Tanzania imelipa zaidi ya Sh milioni 687 baada ya kupewa siku saba na halmashauri hiyo iwe imelipa fedha hizo ambazo zilikuwa za kodi ya pango inazodaiwa na manispaa hiyo.
Fedha hizo zililipwa Desemba 21 na mkataba huo wa zamani unaisha Januari mwakani ambapo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amesema wanaandaa mpya wenye viwango vya malipo vya sasa.
Aidha halmashauri hiyo imeamua kuelekeza fedha hizo ambayo ni sh 687,931,040 katika ujenzi wa vyumba vya madarasa 40 katika halmashauri hiyo kwamba kama itaonekana inawezekana kujenga shule nyingine mpya ya sekondari.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Hapi alisema fedha hizo zimelipwa baada ofisi yake kubaini mchezo mchafu uliokuwa umefanywa na watendaji wa halmashauri yake waliokuwepo huko nyuma ambao walificha mkataba kati yake na Zantel.
Aidha aliipongeza Zantel kwa kutii maagizo waliyopewa na kulipa fedha hizo na tayari wamepewa risiti kuonesha kupokea fedha hizo na kwamba watu wote waliohusika katika jambo hilo watachukuliwa hatua za kisheria. Alisema baada ya malipo hayo, ameelekeza Manispaa kutumia fedha zote hizo kujenga vyumba vya madarasa katika halmashauri hiyo.
“Takwimu zinaonesha mwaka huu watoto 19,000 walifaulu katika Halmashauri ya Kinondoni waliochaguli kujiunga na Sekondari ni 12,889 na hadi sasa wanafunzi 3,169 hawajapata nafasi katika shule zetu kwasababu ya ufinyu wa madarasa,” alisema Hapi. 

Chanzo: ippmedia

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post