Header ads

Header ads
» » Mwanaume mmoja aliyekuwa akikusudia kuuza mtoto amekamatwa na polisi mjini Manchester


Polisi wanasema kuwa wamemkamata bwana huyo mwenye umri wa miaka 28 karibu na soko la Barton Arcade mwendo wa saa nane u nusu majira ya Uingereza.
Polisi wanasema kuwa alikuwa na mtoto msichana anayekisiwa kuwa na miezi 3.
Aidha anasemekana kumuuliza mpita njia iwapo angependa kumnunua mtoto aliyekuwa katika kigari cha kuwakokota watoto.
Polisi waliitwa na mara moja wakamtia mbaroni kwa makosa ya kumtelekeza mtoto.
Mtoto huyo yuko chini ya ulinzi wa serikali na anasemekana kuwa yuko katika hali nzuri kiafya.
Inspekta Liam Boden anasema kuwa watamhoji kuhusiana na madai hayo huku upelelezi wa kina ukianza.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post