Header ads

Header ads
» » Teknolojia:: Kanisa lenye umbo la kiatu Lajengwa nchini Taiwan

 
Kanisa la urefu wa mita 16 lililojengwa kwa kutumia vigae vya glasi linalofanana na viatu vyenye visigino virefu vinavyopendwa sana na wanawake limejengwa huko Taiwan kwa lengo la kuwavutia wanawake zaidi.
Likiwa limejengwa kwa kutumia vigae vya glasi takriban 320,kanisa hilo la rangi ya buluu lina upana wa mita 10 na limegharimu takriban dola 686,000.
Picha iliopigwa juu ya kanisa hilo pia imeonyesha ukubwa wa kanisa hilo pamoja na uzuri wa eneo lililojengwa.
Jumba hilo la kuabudu linatarajiwa kufunguliwa tarehe 8 mwezi Februari tayari kwa mwaka mpya wa Uchina.
 
Kiatu hicho kimetengezwa na maafisa wa baraza la miji kusini magharibi mwa pwani ,katika eneo moja la kitalii lenya umaarufu mkubwa huko Taiwan.
Lakini Pan Tsuei-ping,msimamizi wa ujenzi huo,ameiambia BBC kwamba kanisa hilo halitatumika kwa huduma za ibada za kila siku bali hafla za harusi.

References and useful resources:  
>>BBC NEWS
 
>>Lengo langu ni kuakikisha upitwi na Habari za Teknolojia ungana Nami FACEBOOK , TWITTER na INSTGRAM

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post