Header ads

Header ads
» » Timu ya Queretaro yavunja mkataba wa nyota wa Brazil Ronaldinho

Mkataba wa Ronaldinho wavunjwa

Timu ya Queretaro ya nchini Mexico inaarifiwa kuvunja mkataba wa kiungo wake wa kati kutoka Brazil Ronaldinho.
Katika maelezo yaliyotolewa mtandaoni kupitia tovuti rasmi ya kilabu hiyo, hatua hiyo iliarifiwa kuchukuliwa baada ya maelewano na makubaliano kufanyika kati ya Ronaldinho na Queretaro.
Kilabu ya Queretaro ilitoa shukrani zake kwa Ronaldinho, kutokana na mchango wake aliotoa tangu mwezi Septemba mwaka jana alipojiunga.
Kwa sasa Ronaldinho mwenye umri wa miaka 35 anafuatiliwa na kilabu ya Antalyaspor inayocheza kwenye ligi kuu ya Spor Toto Super League nchini Uturuki.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Wachezaji wa Jamaica walipoza maumivu ya kufungwa kwa kupiga picha za selfie na Lionel Messi
»
Previous
Google yakubali kuondoa picha zote za uchi