Header ads

Header ads

headlines

    3:02 PM J
» » Wachezaji wa Jamaica walipoza maumivu ya kufungwa kwa kupiga picha za selfie na Lionel Messi



Mashindano ya Copa America ya mwaka 2015 yaligeuka na kuwa maonyesho ya picha  baada ya mechi kati ya Argentina na Jamaica kukamilika.
Jamaica walishindwa 1 – 0 na Argentina na kulazimika kufunga virago baada ya kushika mkia katika kundi B bila pointi yoyote.
Licha ya huzuni uliotanda miongoni mwa mashabiki wa Jamaica kutokana na kubanduliwa kwenye mashindano hayo, wachezaji wa Jamaica walichukuwa fursa hiyo kupiga picha za selfie na nyota wa Argentina Lionel Messi punde tu refa alipopuliza kipenga cha mwisho.

Ushindi huo dhidi ya Jamaica uliiwezesha Argentina kumaliza katika nafasi ya kwanza kwenye kundi B na kujihakikishia nafasi katika hatua ya robo fainali.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Brazil yatinga robo fainali kombe la Copa America, Colombia yatoshana nguvu na Peru
»
Previous
Timu ya Queretaro yavunja mkataba wa nyota wa Brazil Ronaldinho