Header ads

Header ads
» » » Tanzania kuandaa maonesho ya teknolojia ya kilimo mwezi Januari



Tanzania inatarajiwa kuandaa maonesho ya wazi ya kilimo yatakayofanyika Januari 26 na 27 mwakani katika mji wa Arusha.
Maonesho hayo yanayojulikana kama "Maonesho ya teknolojia ya kilimo ya Tanzania" yatawaleta pamoja wakulima, maofisa, mashirika ya kilimo, mashirika yasiyo ya kiserikali, watafiti, wafanya biashara, pamoja na wawekezaji na wanabenki.
Akiongea kuhusu maonesho hayo, mshauri wa mambo ya sera katika wizara ya Kilimo, mifugo na uvuvi David Nyange amesema teknolojia zitakazoonyeshwa zina uwezo wa kubeba jukumu kubwa kuelekea kilimo cha kibiashara.
 
Maonesho hayo ya wazi yalianzia katika kituo cha kilimo cha Chisamba nchini Zambia miaka mitatu iliyopita, na yametoa msukumo mkubwa katika sekta ya kilimo nchini humo

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post