Fluminense ilitangaza habari hii kupitia mtandao wa kijamii wa twitter ambapo walisambaza picha za Ronaldinho akiwa na jezi nambari kumi ya timu hiyo.
Ronaldinho alisalia bila timu baada ya kuondoka kutoka kilabu cha Queretaro cha Meksiko mwezi uliopita.
Mkongwe huyu wa Brazil anakumbukwa sana kutokana na mchango wake katika timu ya taifa ya Brazil iliyotwaa kombe la dunia mwaka wa 2002 na pia kwa kipindi chake akiwa na Barcelona.
Ronaldinho alianza soka katika timu ya Gremio kabla ya kuchezea PSG, Barcelona na AC Milan.