Header ads

Header ads
» » Serbia yashinda kombe la dunia la vijana wasiozidi umri wa miaka 20 kwa mara ya kwanza

Serbia yashinda kombe la dunia kwa mara ya kwanza

Mashindano ya FIFA ya kombe la dunia la vijana wasiozidi umri wa miaka 20 yaliyoandaliwa nchini New Zealand, yalifkia kileleni kwa mechi ya fainali na ile ya kuwania nafasi ya mshindi wa tatu.
Timu ya Brazil ilichuana na Serbia kwenye fainali ya kuwania kombe la dunia ilihali wawakilishi kutoka barani Afrika Senegal na Mali, wakatoana jasho kugombania nafasi ya mshindi wa tatu.
Brazil na Serbia zilitoka sare ya 1 – 1 katika muda wa kawaida na kulazimika kucheza katika kipindi cha muda wa ziada ili kuabinisha mshindi.
Hatimaye Serbia walipata goli la ushindi katika muda wa ziada lililofanya mechi hiyo kumalizika 2 – 1 na kubeba ubingwa wa kombe la dunia kwa mara ya kwanza katika historia.
Na katika mechi ya mshindi tatu, timu ya Mali ilifanikiwa kumaliza wa tatu baada ya kuicharaza Senegal bao 3 – 1.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post