Header ads

Header ads
» » Tanzania yazindua kampeni mpya ya kupambana na uwindaji haramu wa wanyama pori

Kampeni mpya ya kulinda wanyama pori Tanzania

Serikali ya Tanzania imezindua kampeni mpya ya kuelimisha jamii kuhusiana na tatizo la uwindaji haramu wa wanyama pori lililokita mizizi nchini humo.
Kampeni hiyo ilizinduliwa rasmi na Waziri wa Maliasili na Utalii wa Tanzania Lazaro Nyalandu, akishirikiana na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, mashirika ya wanyama pori pamoja na msanii maarufu wa muziki nchini humo Alikiba.
Kampeni hiyo inalenga kuielimisha jamii na kuihamasisha kujiunga katika mapambano dhidi ya uwindaji haramu wa wanyama pori kama vile ndovu na wengineo.
Waziri Nyalandu alisema kuwa ndovu ni mojawapo ya vivutio vikubwa vya watalii nchini Tanzania na sekta ya utalii inachangia asilimia 17 ya mapato ya kitaifa.
Msanii wa muziki Alikiba ambaye aliteuliwa kuwa balozi wa kampeni hiyo, alidhihirisha azma yake ya kutaka kuwajibika kikamilifu kwa ajili ya kulinda wanyama pori.
Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazotambulika kote duniani kwa mbuga zake za wanyama pori zinazovutia watalii wengi. Hata hivyo katika kipindi cha miaka 6 iliyopita., nchi hiyo imepoteza asilimia 60 ya ndovu waliowindwa kwa ajili ya biashara haramu ya pembe.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post