Header ads

Header ads
» » Kampuni ya Huawei inasifika kwa kuunda bidhaa ngumu na imara

Kampuni ya Huawei inasifika kwa kuunda bidhaa ngumu na imara TeknoTaarifa imebaini hilo kupitia matukio haya.
Simu ya Huawei P8 Lite ilipookoa uhai wa mwanaume wa miaka 41 pale alipovamiwa nje tu ya nyumba yake, Alipigwa risasi ambayo kwa bahati tuu ilipiga kwenye simu yake ya Huawei iliyokuwa kwenye mfuko wa koti lake.

 
Simu hiyo ya Huawei P8 Lite ilikuwa na ubora wa kutosha kuweza kutoruhusu risasi hiyo kupenya kwa urahisi na kuingia kwenye mwili wake. Risasi ilinasa ndani ya simu.
Simu ya Huawei P8 Lite yenye ukubwa wa inchi 5 inakijumba cha plastiki (housing) na inapatikana kwa takribani Tsh laki 4.
Habari ya tukio hili iliandikwa kwa kujivunia sana huko nchini China. Wakifurahia kuona ubora wa bidhaa zao. 


Huawei walimpa zawadi ya simu nyingine Bwana Abrahams baada ya kupata taarifa kuhusu tukio hilo.

Hii si mara ya kwanza kwa kifaa cha Huawei kuokoa uhai wa mtu. Tovuti ya QZ.com inasema mwaka 2013 nchini Kenya, mtafiti Dennis Mbuvi naye alinusurika kifo baada ya risasi kunasa kwenye tableti yake ya Huawei.
Simu za viwango vya juu kutoka Huawei zimeanza kukubalika kwa kasi katika mataifa ya Ulaya na ata Marekani. Kuna mtazamo ya kwamba kwa sasa viwanda vinavyoweza kutengeneza bidhaa zenye ubora wa kimataifa.

Imehaririwa na;- Unknown

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post