Kwa mujibu wa video hiyo, Facebook imeongeza hisia za uso kwenye kitufe chake cha ‘Like’.
Maboresho hayo yameibuka siku chache baada ya Facebook kutangaza mpango wake wa kuweka kitufe cha ‘Dislike.’
Kulingana na maelezo ya Zuckerberg, Facebook inasemekana kupendekeza maboresho hayo ili kuwawezesha watumiaji kujieleza hisia zao kuhusiana na ujumbe au kitu chochote kitakachosambazwa mtandaoni.