Kuna taarifa kuwa chanzo cha kifo cha ghafla cha rapper Mangweir ni
kuzidisha madawa ya kulevya aliyotumia usiku wa kuamkia leo. Inadaiwa
kuwa Mangwea alikuwa pamoja na mtu aitwaye M TO THE P ambaye naye yupo
mahututi kwa sasa.

Hata hivyo mwenyeji wa rapper Albert Mangwea aliyefariki leo jijini
Johannesburg nchini Afrika Kusini, amesema hit maker huyo wa Mikasi
amefariki akiwa usingizini.

Akiongea na Clouds FM muda mfupi uliopita, mwenyeji huyo aitwaye
Jonathan amesema usiku wa kuamkia leo Mangwair alirudi nyumbani
alikofikia akiwa mzima wa afya lakini mpaka kunakucha hakuonesha dalili
za kuamka.
“Sijui hata huko alitumia nini,” amesema.
Ameongeza kuwa asubuhi kulipokucha aliondoka kuendela na mishemishe
yake na alipokuwa huko wenzake walimpigia simu kumtaarifu kuwa
wamempeleka hospitali ya St. Helen ya jijini humo kwakuwa alikuwa bado
hajaamka na ndipo walipogundua kuwa ameshafariki.
Hata hivyo amesema hakuweza kujua sababu za kifo cha Ngwair kwakuwa
maelezo ya daktari yalikuwa kitaalam kiasi cha kushindwa kuelewa. Ngwair
alikuwa amepanga kurudi leo nchini.
Awali Bongo5 ilizungumza na Bushoke anayeishi jijini Pretoria ambaye
amesema alikuwa akutane naye leo jijini Johannesburg lakini alishangaa
kutompata kwenye simu. Amesema baada ya kuwatafuta washkaji ambao ni
wenyeji wake ndipo walipomuambia kuwa Ngwair amefariki.
“Unajua Ngwair ni mshkaji wangu sana yaani hata siamini kama amefariki aisee,” amesema Bushoke.
Bushoke amesema kesho amepanga kwenda Johannesburg kujionea mwenyewe.
Taarifa za kifo cha Ngwair zimepokelewa kwa mshtuko na watu na
makampuni mbalimbali nchini yametuma salamu za rambi rambi kupitia
kwenye mitandao ya kijamii.
Kilimanjaro Lager
Umeondoka wakati bado tasnia ya muziki inakuhitaji. Pumzika kwa Amani Albert Mangwea “Cowwizy”.
Ndovu Special Malt
R.I.P Albert Mangweir! You will be missed by many Tanzanians.
Adam Nditi
Yani siamini Mangwear amefariki dunia nini ilichomkuta #RIP #Mangwair #akaCowbama
Diva
Jamani Ngwair , am in tears now ….. Jamani!. I can’t believe this. I can’t tweet The RIP….. Whyyyyy?
Home
»
»Unlabelled
» HIKI NDICHO ALICHOKISEMA BUSHOKE AKIWA SOUTH AFRIKA KUHUSU KIFO CHA NGWAIR, SOMA HAPA
Topics:
Imehaririwa na;- poatel Africa
Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
THE UNITED DEPUBLIC OF TANZANIA MINISTRY OF HOME AFFAIRS EMPLOYMENT OPPORTUNITIES The Ministry of Home Affairs in clos...
-
Mambo vipi Rafiki yangu? Kama wewe ni miongoni mwa watu wanaopendelea kuweka Pattern kwenye simu zenu kwa usalama zaidi, Basi msijali...
-
BEST TANZANIAN UNIVERSITIES 2015: Latest Rankings 23 February 2015. A list of best universities has just gotten out and the result i...
-
The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) is a Government Institution which is under the Ministry of Education and Vo...
-
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kuanzia tarehe 1...
-
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo kilichowekwa kanisani wakati wa mazishi ya kada mkongwe wa CCM Mzee...
-
Mwana wa Sokwe anaendelea vyema baada ya kuzaliwa kupitia upasuaji katika hali isiyo ya kawaida. Sokwe huyo anayetoka upande wa magha...
-
Ref. Na EA.7/96/01/H/ 66 07th August, 2015 VACANCIES ANNOUNCEMENT On behalf of Eastern Africa Statistical Training Centre ...
Data Boosta
Ungana nasi Facebook
PPF FUND