Header ads

Header ads
» » Facebook ina mpango wa kuzindua satalaiti Afrika

 

Facebook ina mpango wa kuzindua satalaiti Afrika ili kupanua upatakanaji wa huduma za Internet barani humo

Facebook ikishirikiana na huduma ya Mawasiliano ya Ufaransa Eutelsat itaanzisha mradi wake kuzindua satalaiti Afrika ili kupanua upatikanaji wa Internet hasa maeneo makubwa ya Afrika Kusini na Sahara.
Satalaiti hiyo ni mojawapo ya sehemu ya Facebook ya Internet.org na itatumika hasa katika upatikano wa mtandao kwa simu za mkononi,tayari shughuli za  ujenzi wa satalaiti hiyo unaendelea na uinduzi unatarajiwa kufanyika mwaka 2016.
Mkurugenzi mkuu wa Facebook Mark Zuckerberg alifahamisha kwamba satalati hiyo inayojulikana kwa jina AMOS-6,itafikisha huduma zake magharibi,mashariki na kusini mwa Afrika.
Facebook ina watumiaji milioni 20 kutoka nchi za masoko makuu kutoka Afrika;Nigeria na Kenya na takwimu zaonyesha kuwa wengi wa watumiaji hutumia simu za rununu.
Aidha kampuni hiyo ilifungua ofisi yake ya kwanza Afrika jijini Johannesburg mnamo mwezi Juni mwaka huu.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post