VIJANA watatu wanaoaminika kuwa ni wafuasi wa chama kikuu cha
upinzani CHADEMA, wamekamatwa na polisi eneo la Magomeni Mapipa jijini
Dar es Salaam leo Ijumaa Januari 2, 2014, baada ya jaribio lao la
kufanya matembezi kutoka mkoa wa Geita wakielekea Ikulu ya Dar es Salaam
kumuona Rais Jakaya Kikwete kufikisha malalamiko yao.
Kwa mujibu
wa taarifa ya Mkuu wa Wilaya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Jordan
Rugimbana, vijana hao watatu, Juma Maganga, Khalifa Selemani na Athanas
Michael, walielekezwa na maafisa usalama kumuona yeye DC baada ya
kuwasili kwenye eneo lake la utawala wakitokea Geita, ili awape baraka
za kwenda Ikulu.
Lakini walipofika ofisini hapo, DC huyo alitaka kujua
nini hasa kilichowafanya watembee safari ndefu kama hiyo?