Header ads

Header ads
» » KUTANA NA MSICHANA ALIYENUSULIKA KATIKA AJARI YA NDEGE



Ajali ya ndege
Mtoto mmoja wa miaka saba ametembea hadi katika nyumba moja katika jimbo la Kentucky nchini Marekani ili kuripoti kuanguka kwa ndege aliyoabiri.
Kulingana na polisi ndege hiyo baadaye ilipatikana imeanguka huku watu wanne wakiwa wamefariki katika kaunti ya Lyon yapata kilomita 50 mashariki mwa mji wa Paducah
Kituo cha runinga cha NBC nchini Marekani kimesema kuwa msichana huyo alimwarifu mtu aliyemfungulia mlango kwamba wazazi wake walifariki katika ajali hiyo ya ndege.
Picha ya ndege hiyo haijatolewa na polisi hawajatoa tamko lolote kuhusu uhusiano wake na waathirwa.
Shirika linalosimamia anga za juu limesema kuwa maafisa wanaodhibiti usafiri wa ndege walipoteza mawasiliano na ndege hiyo aina ya Piper PA-34 baada ya rubani kuripoti matatizo ya mitambo.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post