Header ads

Header ads
» » Kenya imechukuwa uamuzi wa kujenga ukingo mpakani mwake na Somalia

Kenya kujenga ukingo mpakani mwake na Somalia

Ili kukabiliana na mashambulizi kutoka kwa wanamgambo wa al shabaab, Kenya imechukuwa uamuzi wa kujenga ukuta na kuuzungushia nyaya za umeme eneo la kilomita 700 mpakani mwa Kenya na Somalia.
Wizara ya mambo ya ndani nchini Kenya ikiongozwa na Salim Mahmoud ilifahamisha kuwa kundi la wahandisi linafanya utafiti kuhusu hali ya ardhi ya eneo hilo ili kufahamu kiwango cha vifaa vya ujenzi vitakavyo hitajika.
Baada ya utafiti huo, shughuli za ujenzi zitaanzishwa mara moja.
Ukingo huo unatarajiwa kujengwa bain aya Lamu na Wajir.
Shuhuli za ujenzi zitaanza ifikapo mwezi Julai.
Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani, Mwenda Njoka alifahamisha kuwa ukingo huo hautokuwa ukuta wa matofali bali nyaya na sinyenge ambazo zinakuwa na umeme.
Mradi wa kujenga ukingo huo umeharakishwa kutokana na kuuawa kwa wanamgambo 11 wa el shabaab Lamu wakitokea Somalia.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Star wa Bongo Movie Mwingine Huyu Hapa Anaehitaji kuingia Bungeni
»
Previous
Alichopost davido kuhusu watanzania na comment ya wema sepetu