Header ads

Header ads
» » Simu ya kwanza inayoweza kuoshwa kwa Maji na sabuni

DIGNO Rafre Is The First Phone You Can Wash With Soap
Mambo vipi Rafiki? Naamini wengi wetu tunaamini simu zetu zikiingia maji basi litakuwa tatizo lakini kwa jinsi Teknolojia inavyozidi kukua kila kukicha, ndivyo tunavyozidi kupata vitu vya aina mbalimbali na vya kustajabisha, kama simu hii ya kwanza kutengenezwa ambayo inaweza kuoshwa na sabuni, simu hiyo iliyotengenezwa na kampuni ya kijapani ya KDDI simu hiyo inayo kwenda kwa jina la “Digno rafre” inategemewa kuzinduliwa siku chache zijazo. Ndio zipo simu janja nyingi ambazo zinauwezo wa kuzuia maji kuingia ndani ya simu lakini hii itakuwa ni simu ya kwanza ambayo itaweza kusio tu kuzuia maji kuingia ndani bali hata kama utataka kuiosha na sabuni basi utaweza kufanya hivyo bila kuwa na wasi wasi na kuiharibu. 
 Face It, You’ve Always Wanted to Wash Your Phone with Soap and Water. Now You Can
Simu hiyo inayotegemewa kuuzwa kwa karibu dola 175 za kimarekani (Takribani laki nne za sh) na pengine itauzwa Japani tu kwa sasa. Watengenezaji wa simu hii wanawalenga hasa wazazi ambao wanawatoto wadogo ambao ni rahisi kuchafua simu zao. Simu hiii hata hivyo itaweza kuhimili kuoshwa na baadhi ya sabuni sio kila sabuni, katika tangazo ambalo watengenezaji wa simu hiyo wameliweka mtandaoni mtoto 
anadondosha simu katika chakula na mama yake anaonekana akiiosha katika bomba na sabuni kisha baadaye mtoto anaonekana akichezea simu bafuni. Teknoloji inayotumika hapa ni ile ya kuzuia maji kuingia ndani ya simu lakini imeongezwa pia uwezo wa kuzuia povu na sabuni, screen yake kwa upande mwingine ni kwamba inaweza kutumiwa hata na mikono mibich
TAZAMA VIDEO HAPA


References and useful resources:  
 >techlomedia

>>>Tafadhali Click link zifuhatazo kuhungana Nami FACEBOOK , TWITTER na INSTGRAM 

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post