Header ads

Header ads
» » Mke wa Kagame awataka wasichana wa Kiafrika kusomea taaluma ya mawasiliano na teknolojia (ICT)

Mke wa Kagame ahimiza wasichana wasomee ICT

Mke wa rais wa Rwanda Bi. Jeannette Kagame, ametoa wito kwa wasichana wa Kiafrika kujihusisha na taalum ya mawasiliano na teknolojia ili kupewa nafasi katika ulimwengu wa kisasa.
Akihutubia kwenye mkutano wa maendeleo ya Afrika, Bi. Jeannette Kagame alihimiza wasichana wa Kiafrika kuzingatia masomo ya kompyuta ili kuchangia maendeleo ya teknolojia barani Afrika.
Bi. Jeannette Kagame alibainisha kuachwa nyuma kwa wasichana na wanawake wengi wa Kiafrika kutokana na ukosefu wa elimu ya ICT.
Rwanda imekuwa ikifanya kampeni za kuboresha taaluma katika nyanja za sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati.
Mnamo mwezi Agosti, Rwanda iliandaa kongamano maalum la wiki tatu ambapo wanafunzi wa kike 120 kutoka Ethiopia, Ghana, Kenya, Nigeria, Afrika Kusini, Tanzania, Uganda na Marekani walihudhuria.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post