Header ads

Header ads
» » Familia ya Messi ilishambuliwa na mashabiki wa Chile katika mechi ya fainali

Familia ya Messi yashambuliwa katika mechi ya fainali

Mama na ndugu zake Messi walilazimika kutazama mechi ya fainali kwenye runinga baada ya kushambuliwa na mashabiki wa Chile

Kando na mbwembwe za kushinda kombe la Copa Amerika kwa mara ya kwanza, mashabiki wa Chile waliitia aibu nchi yao waliposhambulia familia ya mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi.
Dakika kadhaa kabla kipindi cha mapumziko kaka mkubwa wa Messi, Rodrigo aligongwa na kitu kilichotupwa na mashabiki wa Chile jambo lililopelekea kuondoshwa kwa familia hiyo kutoka eneo la mashabiki.
Messi kwa mara nyingine alishindwa kuiongoza Argentina kufikia taji baada ya kulemewa katika mikwaju ya penalti.
Chile waliandikisha historia kwa kutwaa kombe hilo kwa mara ya kwanza.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post