Header ads

Header ads
» » Michezo ya Commonwealth 2022 kufanyika barani Afrika


Durban itakuwa mji wa kwanza Afrika kuwa mwenyeji wa michezo ya 'Commonwealth' mwaka 2022.
Jiji la Durban ni mojawapo ya miji iliyopo katika pwani ya Afrika Kusini.
Uamuzi huo ulitolewa baada ya mkutano mkuu uliofanywa na  maafisa wa mashirika ya kufanikisha tamasha hiyo ya michezo nchini New Zealand.

Mkuu wa shirika la CGF Prince Tunku Imran alisema “Ni ufahari mkubwa kwa Afrika baada ya Durban kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa michezo ya 22 ya Commonwealth”.
Michezo ya Commonwealth hufanyika kila baada ya miaka nne na wanariadha hutoka kwa zaidi ya nchi 50 wengi wao wakiwa raia wa nchi zilizokuwa chini ya ukoloni wa Uingereza.
Michezo ya Commonwealth kwa mara ya kwanza yalifanyika mwaka 1930.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Kondoo wa Australia aweka rekodi ya dunia kwa uzito wa kilo 42.3 za pamba mwilini
»
Previous
adaiwa kumtoroka mumewe na kwenda kuchumbiwa