Header ads

Header ads
» » Magoli Matatu kutoka kwa IVAN RAKITIC, SUAREZ na NEYMAR yaliipa Barcelona taji lake la tatu msimu huu

 Barcelona yanguruma Ulaya, yatwaa ubingwa kwa kishindo

Barca ilitinga uwanjani ikiwa tayari ina taji la kombe la ligi kuu nchini Hispania na taji la kombe la mfalme yaani Copa del Rey.
Ushindi wa leo dhidi ya Juventus ya Italia, umemaanisha kuwa kocha Luis Enrique ameivunja rekodi ya Pep Guardiola ya kuzoa makombe matatu katika msimu wa awali klabuni hapo.
Goli la kwanza la Barcelona lilifungwa mnamo dakika ya tano ya mchezo baada ya Rakitiç kumalizia pasi safi kutoka kwa Iniesta.
Goli hilo lilidumu hadi mapumziko
Morata alirudisha matumaini ya Juventus baada ya kusawazisha goli hilo punde tu walipotoka mapumziko.
Kusawazishwa kwa goli hilo kulinyanyua ari na morari ya Barcelona ambayo iliwatumia vyema Suarez na Neymar kupigilia misumari mingine miwili.
Hongera kwa Barcelona ambao ni mabingwa wapya wa klabu bingwa barani Ulaya maarufu kama UCL.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post