Header ads

Header ads
» » Hii ndiyo Teknolojia ya Buggati Veyron Gari lenye gharama kubwa zaidi Duniani



Bugatti Veyron Super Sports ndio gari iliyo ghali kuliko zote Duniani ambapo gari hiyo imeuzwa moja tu kwa toleo la mwaka 2012. Tuanze na bei gari hii toleo la Super Sports ni US$ 2,400,000 sawa na Shillingi za Tanzania karibu trilioni tatu nukta tisa.
Kwa upande wa kasi gari hiyo ina uwezo wa kutoka 0 hadi 60 kph kwa muda wa sekunde 2.5 na pia hufikia kasi ya 200 kph kwa muda wa sekunde 7.3 yaani muda huu ni kuanzia kuwa gari imesimama. (kutoka sifuri). Kasi ya ya juu kabisa ya gari hiyo ni 430 kph, yaani ina kasi kuliko hata gari za Formula One. 
Hadi mwaka jana takwimu zinaonyesha kwamba idadi kamili ya gari hizo zilizouzwa Duniani ni 12 tu. Kampuni inayotengeneza gari hiyo inakusudia kutengeneza Buggati Veyron nyengine 18 na hivyo kufanya idadi kamili ya gari hizo kuwa ni thelathini tu Duniani. Mmoja wa mmiliki wa gari hii ni mcheza sinema maarufu Tom Cruise ambapo yeye anamiliki Buggati Veyron ambayo sio toleo la Super Sports ambayo huuzwa bei nafuu kidogo yaani US$ 1,700,000 sawa na shilingi trilioni 2.75.
Buggati Veyron Super Sports ina injini yenye kutumia lita nane na ina silinda kumi na sita, injini hiyo ina jumla ya maredieta kumi kwa ajili ya kuipoza. KWa upande wa nguvu injini Buggati Veyron ina jumla ya horse power 1,2000 na turbo charger nne. Gari hii pia ina double difusser exhast system. Buggati Veyron ina uzito wa karibia tani mbili (1.8) 
Kwa upande wa gia; gari hii ina dual clutch, yaani ukitaka unaweza kuiendesha kama manual na ukipenda unaweza kuiendesha kama automatic, ina tanki la mafuta lenye uwezo wa kuingia jumla ya lit 100. Barani Afrika gari hii bado haijawahi kununuliwa.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Peruzi kurasa za Magazeti ya Leo Jumanne Ya Tarehe 24 Juni 2015
»
Previous
UNİCEF yatabili vifo vya watoto milion 68 mpaka ifikapo 2030