Header ads

Header ads
» » Mahakama ya Marekani yaamuru kampuni ya Apple kusaidia FBI

 AppleFBI
Mahakama moja ya Marekani imeamuru kampuni ya Apple kusaidia idara ya upelelezi ya FBI ili kufikia data za simu ya mshukiwa wa ugaidi.
FBI imekuwa ikipeleleza washukiwa wa ugaidi Syed Farook na mkewe Tashfeen Malik wanaodaiwa kutekeleza mashambulizi tarehe 2 Desemba mwaka jana katika mji wa San Bernardino, California.

Washukiwa hao wawili wanadaiwa kuua watu 14 kwa kuwafyatulia risasi kabla ya kuuawa na polisi.
Jaji wa mahakama hiyo Sheri Pym alitaarifu kampuni ya Apple baada ya FBI kushindwa kufikia data za simu hiyo aina ya iPhone iliyokuwa imefungwa na nywila ya siri.
Kwa kawaida idara ya FBI ina utaratibu wa kuchunguza kwa undani vifaa vyote binafsi vilivyokuwa vikitumiwa na mshukiwa yeyote anayefanyiwa upelelezi.

SOURCE: CNN NEWS

 >>Lengo langu ni kuakikisha upitwi na Habari za Teknolojia ungana Nami FACEBOOK , TWITTER na INSTGRAM

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post