Header ads

Header ads
» » RUNDO LA FEDHA LA MWANGWA BONDE LA MKWAJUNI, mama ntilie watumia kupikia

Fedha chakavu zatupwa jalalani bonde la Mkwajuni.
Fedha chakavu zatupwa jalalani bonde la Mkwajuni.
Mabunda ya fedha zilizoharibiwa na Benki kuu ya Tanzania zimwemwagwa katika Bonde la mkwajuni Kinondoni jijini Dar es salaam na kuzua sintofahamu miongoni mwa wananchi.
Kwa mujibu wa wakazi walioshuhudia fedha hizo wameiambia hivisasa Blog kwamba fedha hizo zipo katika mafungu ya shilingi elfu moja, elfu tano pamoja na elfu kumi.
Inadaiwa kuwa fedha hizo zilianza kuonekana kuanzia jumanne ambapo leo ndio imebainika kwamba zipo kwa wingi katika Bonde hilo.
Kufutia tukio baadhi ya mama ntilie ,Wachoma chipsi wamemiminika katika bonde hilo kuzichukua fedha hizo kwa lengo la kupikia, huku watoto wakizichezea.
Naye mjumbe ambaye haukutaka kutaka jina lake amesema kwamba fedha hizo zinadaiwa kutoka Benki Kuu kwenda kutupwa Bonde la Pugu lakini cha kushangaza zimetupwa katika bonde hilo.
Mamia wa wananchi wamemiminika kwenda katika bonde hilo kujionea  fedha hizo ambapo asilimia kubwa ya wananchi wamesema hawajawahi kuziona fedha nyingi kiasi hicho.
Mtandao wa hivisasa unaendelea kuwatafuta viongozi katika eneo hilo na tutakujulisha kinachoendelea.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post