Tukizungumzia mashine ya kuchapisha vyakula, kwanza tunahitaji kutaja teknolojia ya uchapishaji wa 3D.
Mwaka 1986 Chuo Kikuu cha Uhandisi cha Marekani kilivumbua mashine ya kwanza ya uchapishaji wa 3D, baadaye teknolojia hii ilipata maendeleo ya kasi na kutumiwa katika kazi mbalimbali.
Mwaka 2011, watafiti wa Uingereza walisanifu mashine ya kwanza ya kuchapisha chokoleti. Baadaye kampuni ya Hispania iliboresha teknolojia yao na kutengeneza mashine ya kuchapisha chakula iitwayo Foodini.

Aidha, teknolojia hii inawawezesha watu kuchapisha vyakula vipya kwa kutumia lishe za mwani, majani ya viazi sukari na wadudu, ili kutatua tatizo la ukosefu wa chakula duniani.
Chanzo: dailymail.co.u