Header ads

Header ads
» » Dunia na Visa: Hivi Ndivyo Projector Ilivyomuumbua Profesa aliyekuwa akitizama Video ya ngono darasani

 Projector yamuumbua Profesa aliyekuwa akitizama ngono darasani
Profesa mmoja aliyekuwa akiwasilisha mada katika chuo kikuu cha Wageningen huko Uholanzi, amejikuta katika fedheha ya aina yake mbele ya wanafunzi aliokuwa akiwafundisha baada ya mashine ya kuonyeshea picha (projector) iliyokuwa kwenye ukumbi aliokuwa akifundishia kumuumbua alipokuwa akiangalia picha za ngono.
Profesa huyo ambaye vyombo vya habari vya Uholanzi vimeamua kutolitaja jina lake, alikuwa akifundisha wanafunzi hao kwa kutumia kifaa hicho kilichokuwa kimeunganishwa na kuonyesha somo lake kutokea kwenye laptop yake, na alipomaliza akasahau kuchomoa waya za kuunganisha vifaa hivyo viwili ili aendelee na mambo yake.
Kufuatia hali hiyo, huku akiwa hajui kama wanafunzi wake walikuwa wakifuatilia alichokuwa akikifanya, profesa huyo ambaye anatajwa kuwa ni mtu mzima kidogo kiumri, aliingia kwenye mtandao wa internet na kuanza kufungua site mbalimbali, huku wanafunzi wake wakiwa wanaangalia na kuona alichokuwa akikifanya kupitia projector ya ukumbini hapo.
Lakini wanafunzi hao sio tu kuwa waliendelea kumshangaa profesa huyo, bali mmoja wao alikwenda mbali zaidi kwa kupiga picha na kuipost kwenye mtandao wa kijamii muda huo huo, hali ambayo ilileta tafrani ya aina yake.
Haijajulikana hadi sasa kama profesa huyo atachukuliwa hatua au laa, na ikiwa atachukuliwa hatua, kuwa ni hatua gani zitakazochukuliwa dhidi yake, lakini ni wazi kuwa, tukio hilo litakuwa limemfedhehesha vya kutosha sana.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post