Header ads

Header ads
» » SAMSUNG Yawalipa Wateja walioathiriwa na Galaxy Note 7


Jumatatu hii, Samsung ilianzisha mchakato wa kuwafidia wateja walionunua simu hatari za Galaxy Note 7. Kazi hiyo imeanza Uingereza na Ireland.
Kampuni hiyo imedai kuwa imerekebisha tatizo la betri katika simu hizo, lililosababisha kulipuka na itaanza kuwapa wateja walionunua simu zingine. Uingereza ni nchi ya kwanza kuanza kupokea simu hizo mpya za Note 7.

samsung galaxy note 7 fire
Kwa wateja wa Marekani wataanza kupata simu zao, Jumatano, September 21. Samsung iliingiza Galaxy Note 7 mwishoni mwa August, wiki chache kabla ya kuzinduliwa kwa iPhone 7 ya Apple, mpinzani wake mkuu.
Baada ya simu hizo kuonekana na tatizo la kuchemka, iliziondoa simu hizo sokoni. Kampuni hiyo ilikuwa imetengeneza simu hizo milioni 2.5 na tayari milioni 1 zilikuwa zimenunuliwa.

Imehaririwa na;- Unknown

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post