Tanzania kutumia Programu ya simu ya kupima rutuba ya udongo
Kampuni ya biashara iliyo na makao yake nchini Kenya ya 'Capture Solutions' wiki iliyopita ilitangaza kupanua biashara yake kwa nchi jirani ya Tanzania ikiwa ni pamoja na kuunda programu za simu kwa lengo la kuboresha ukulima nchini.
Mojawapo ya uzinduzi kwa ajili ya wakulima ni kuanzisha programu mpya ya simu za mkononi ambapo wakulima wataweza kupima rutuba ya udongo.
Programu hiyo tayari inatumiwa nchini Kenya na teknolojia hiyo itazinduliwa mapema mwezi wa Septemba jijini Dar es Salaam.
Kampuni hiyo tayari imefungua tawi lake nchini Tanzania .
Programu hio inaweza kutumiwa katika udongo wa aina yoyıte na mahali popote .
Kwa sasa nchini Kenya kuna watu 200,000 waliojisajili na programu za kampuni ya Capture Solutions katika programu hizo kupitia simu aina ya Smartphone .
Chanzo: africanfarming.net