Kampuni ya kutengeneza simu na bidhaa za electroniki kama 'tablet' yafahamisha kufufuka na kutengeneza bidhaa zake upya zitakazouzwa katika soko la kimataifa kwa muda wa miaka kumi.
Nokia ilikuwa kampuni ya simu iliyokuwa inaongoza duniani kati ya mwaka 1998 na 2011 na kuanza kupata hasara baada ya kampuni ya Korea ya Samsung kuingia soko la kimataifa na kutengeneza bidhaa za simu bora zaidi.
Mnamo mwaka 2011 kampuni hiyo ya simu ilitengeneza toleolake la kwanza 'smartphone' ya ''windows ambayo haikuleta mafanikio.
Nokia sasa itashirikiana na Microsoft katika kutoa matoleo mapya ya simu na kuanza uzinduzi mwisho wa mwaka 2016.