Header ads

Header ads
» » Facebook yafanikiwa kufanya majaribio ya ndege isiyo na rubani inayotumia nishati ya jua


Kampuni ya Facebook hivi karibuni imetangaza kuwa imefanikiwa kufanya majaribio ya kwanza ya ndege isiyo na rubani iitwayo Aquila inayotumia nishati ya jua.
Hivi sasa watu bilioni 4 hivi duniani bado hawajaunganishwa na mtandao wa Internet. Mwaka 2014, kampuni hiyo ilianzisha maabara ya uunganishaji, ambayo inalenga kutoa huduma ya mtandao wa Internet kupitia ndege zisizo na rubani, satilaiti na mifumo ya mawasiliano ya simu


Tarehe 28 maabara hiyo ilifanya majaribio ya kwanza ya ndege ya Aquila huko Arizona, Marekani. Kiunzi cha ndege hii kilitengenezwa kwa nyuzi za kaboni, upana wa mabawa yake ni mkubwa kuliko ndege ya abiria ya Boeing 737, lakini uzito wake ni theluthi moja ya gari la nishati ya umeme. Ndege hiyo inaweza kuruka angani kwa miezi mitatu mfululizo, lakini inatumia nishati chache tu ambayo ni sawa na nishati inayotumiwa na vyombo vitatu vya kukausha nywele au maikrowevu moja.
Kwa mujibu wa mpango, ndege hiyo inaweza kuzunguka eneo lenye kipenyo cha kilomita 97, na kutoa ishara ya mtandao wa Internet kutoka anga yenye urefu wa kilomita 18 kwa mifumo ya mwangaza leza na mawimbi ya masafa ya milimita. 


Chanzo: technewstoday.com

Imehaririwa na;- Unknown

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post