Kampuni ya Facebook hivi karibuni imetangaza kuwa imefanikiwa kufanya
majaribio ya kwanza ya ndege isiyo na rubani iitwayo Aquila inayotumia
nishati ya jua.
Hivi sasa watu bilioni 4 hivi duniani bado
hawajaunganishwa na mtandao wa Internet. Mwaka 2014, kampuni hiyo
ilianzisha maabara ya uunganishaji, ambayo inalenga kutoa huduma ya
mtandao wa Internet kupitia ndege zisizo na rubani, satilaiti na mifumo ya mawasiliano ya simu
Tarehe 28 maabara hiyo ilifanya majaribio ya kwanza ya ndege ya Aquila
huko Arizona, Marekani. Kiunzi cha ndege hii kilitengenezwa kwa nyuzi za
kaboni, upana wa mabawa yake ni mkubwa kuliko ndege ya abiria ya Boeing
737, lakini uzito wake ni theluthi moja ya gari la nishati ya umeme.
Ndege hiyo inaweza kuruka angani kwa miezi mitatu mfululizo, lakini
inatumia nishati chache tu ambayo ni sawa na nishati inayotumiwa na
vyombo vitatu vya kukausha nywele au maikrowevu moja.
Kwa mujibu wa
mpango, ndege hiyo inaweza kuzunguka eneo lenye kipenyo cha kilomita 97,
na kutoa ishara ya mtandao wa Internet kutoka anga yenye urefu wa
kilomita 18 kwa mifumo ya mwangaza leza na mawimbi ya masafa ya
milimita.
Chanzo: technewstoday.com
Home
»
HABARI TECH
» Facebook yafanikiwa kufanya majaribio ya ndege isiyo na rubani inayotumia nishati ya jua
Topics: HABARI TECH
Imehaririwa na;- Unknown
Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
Wachezaji wa Yanga wakifanya mazoezi jana jioni kwenye uwanja wa Mbegani, Bagamoyo Timu ya Yanga SC jana imekamilisha kujifua kwa m...
-
BEST TANZANIAN UNIVERSITIES 2015: Latest Rankings 23 February 2015. A list of best universities has just gotten out and the result i...
-
WATU wawili, Said Abdallah (37) na Ally Mwishee (44), wameuawa kwa kupigwa risasi na kufa papo hapo katika uwanja wa mpira wa miguu wa ...
-
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA Kumb. Ref. Na EA.7/96/01/H/41 ...
-
mabingwa hao watetezi wa ligi kuu ya Premia ya Uingereza walipokuwa wakikabiliana na Swansea jana usiku huku wakiwa na mchezaji mmo...
-
Kama ndo machine aliyo nunua safari hii basi katisha aisee maana hii ni one of the most expensive and luxury cars around na hela ya...
-
The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) is a Government Institution which is under the Ministry of Education and Vo...
-
He trusts lions enough to stick his arm in their mouth! Kevin leverages his ability to help prevent these...
-
JOB VACANCY Precision Air Services Plc is a fast growing private Tanzanian airline which operates in Partnership with Kenya Air...
-
Mshambuliaji matata wa Barcelona na kapteni wa Argentina Lionel Messi,...