Wanafunzi wa shule ya msingi Butere katika kaunti ya Kakamega walikuwa mojawapo ya wanafunzi wa kwanza nchini Kenya kupata vipakatilishi au 'Laptop'.
Hadi kufikia sasa takriban shule 150 za msingi za mijini na vijijini zimepata vipakatilishi hivyo kutoka kwa serkali .
Mfumo wa kusoma kwa kutumia laptop hizo zitahamasisha ujuzi na pia kazi za pamoja katika maisha ya wanafunzi katika shule za msingi nchini Kenya.
Mradi huo ni ahadi iliyotolewa na chama cha Jubilee wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2013.
Kuchelewa kwa kutimiza ahadi hiyo kumekosolewa vikali na upinzani nchini humo wakidai Jubilee hawatimizi ahadi zao
Chanzo: standardmedia.co.ke