Header ads

Header ads
» » Njia inayotumia facebook kuingiza Pesa, Kupita watumiaji wake


Facebook ambayo kwa sasa inapatikana katika lugha 70 ulimwenguni, ni mtandao wa jamii ambao unaongoza kwa kuwa na watumiaji wengi zaidi duniani. Wewe na mie kama watumiaji wa Facebook tunainufaisha kampuni hiyo ya Facebook, kwani kupitia kuitumia kwetu kunaiwezesha Facebook kuingiza mapato kwa njia ya moja kwa moja au nyingine.

Makala hii inakuchambulia namna ambavyo Facebook inaingiza "vijisenti" vyake:-



1. Kupitia Matangazo: Kwakuwa inao watumiaji wa mtandao wengi, ni rahisi kwa Facebook kushawishi watu binafsi na makampuni kutangaza bidhaa zao kupitia aina mbalimbali za matangazo yanayorushwa hewani na Facebook. Mfano , kampuni inaweza kudhamini POST yake, ili ionekane kwa watu wengi zaidi na mara nyingi. Pia kuna matangazo ya biashara ambapo unaweza kutengeneza tangazo lako la biashara na kulirusha hewani kupitia Ukurasa wako wa Facebook (Facebook Page).  Ili kutengeneza tangazo Facebook, unaweza kuenda sehemu maalum ukiwa Facebook imeandika CREATE AN AD.

Unahitaji kuwa na Credit Card au Umejisajili na unayo akaunti ya Paypal ili kuweza kulipia huduma hii.
Mfano wa matangazo yanayoingizia Facebook 'vijisenti'
Namna nyingine kampuni ya Facebook inavyoingiza 'vijisenti'
2. Salio maalum la Facebook ( Facebook Credit)

Ni kama vile unavyonunua salio la simu yako ili utumie salio hilo kupiga simu, ila kwa Facebook, unaponunua Facebook Credit, ni kwa ajili ya kuweza kutumia credit hiyo kulipia kucheza Games, au hata kununua vitu katika baadhi ya maduka yanayouza bidhaa zao ndani ya Facebook.

Unahitaji kuwa na Credit Card au Umejisajili na unayo akaunti ya Paypal ili kuweza kununua Facebook Credit.
Sehemu ya Games ndani ya Facebook, baadhi ya Games inabidi ulipie, na unaweza tumia Facebook Credits kulipia.


3. Kupitia Kuudha bidhaa mbalimbali

Facebook inayo huduma ya kuuza bidhaa mbalimbali kwa mtindo wa "Gift" ambapo wewe mtumiaji unachagua nani unataka kumnunulia bidhaa , kisha unaenda kwa profile ya huyo unayetaka kumuuzia bidhaa. Utaona sehemu imeandikwa GIVE GIFT, ukibofya hapo utakutana na aina mbalimbali za zawadi na maelekezo. Hata hivyo huduma hii ya kutoa zawadi kwa watu haipataki kwa kila nchi. Inabidi ucheki Profile ya mtu husika unayetaka kumpa zawadi kuona kama GIVE GIFT ipo katika profile yake.
 

>>Lengo langu ni kuakikisha upitwi na Habari za Teknolojia ungana Nami FACEBOOK , TWITTER na INSTGRAM

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post