Apple iPhone 6S kuzinduliwa rasmi tarehe 9 Septemba nchini Marekani
iPhone S6 itazinduliwa rasmi kwenye maonyesho ya Apple yatakayoandaliwa tarehe 9 Septemba katika mji wa San Francisco nchini Marekani.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa, simu ya iPhone S6 inasemekana kuwa na muundo unaofanana na iPhone nyinginezo ingawa itakuwa na maboresho makubwa ya kiteknolojia.
iPhone 6S itakuwa na skrini ya mfumo wa Force Touch, kamera ya ubora wa 12 MP, mfumo wa A9 Chipset, RAM ya 2 GB nna betri lenye uwezo wa kudumu kwa masaa mengi.