Header ads

Header ads
» » Polisi wakamata tani 1 ya madawa ya kulevya uwanja wa ndege wa kimataifa nchini Colombia

Operesheni dhidi ya madawa ya kulevya Colombia

Polisi wa Colombia wamekamata tani moja ya madawa ya kulevya yaliyokuwa ndani ya ndege ya kusafirisha shehena katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa El Dorado ulioko Bogota.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa, madawa hayo ya kulevya yalikuwa yamefichwa ndani ya viroba 40 na kufunikwa kwa kemikali ya Zinc Oxide kwenye ndege ya shehena aina ya AM0762 inayomilikiwa na shirika la ndege la Copa Airlines.
Video iliyorekodiwa na kamera za siri ilionesha viroba 40 vilivyokuwa na madawa ya kulevya yaliyofungwa ndani ya paketi ndogo za plastiki.
Hakuna mhusika yeyote wa ulanguzi wa madawa ya kulevya aliyetiwa mbaroni katika operesheni hiyo ingawa ripoti zinaashiria kwamba madawa hayo yalitoka kwa walanguzi wa Bogota na Cartagena waliokuwa na uhusiano wa kibiashara na Mexico.
Maafisa wakuu wamearifu kwamba madawa ya kulevya yalipangwa kusambazwa Marekani na Ulaya kupitia Marekani ya Kati.
Mnamo wiki jana, polisi wa Mexico pia waliwahi kukamata kilo 961 za madawa ya kulevya katika operesheni yao.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post