Header ads

Header ads
» » watu tisa (9) wamekufa kutokana na athari za Kimbunga nchini China

 
Utawala wa jimbo la Zhejiang lililoko Mashariki mwa China umethibitisha vifo vya watu 9 kutokana na athari za kimbunga kinachoendelea kuponda pwani yake.
Maafisa wanasema kuwa Mafuriko ,tope zito na maporomoko ya ardhi yamekumba maeneo hayo baada ya mvua kubwa ikiandamana na upepo mkali kulikumba eneo hilo.
Maelfu ya watu wamelazimishwa kuhama makwao kufuatia mvua kubwa iliyoleta hatari ya kutokea mafuriko.
Katika maeneo yaliyoko chini karibu na bahari kumeripotiwa mvua kubwa takriban centimita 50 katika kipindi cha saa ishrini na nne zilizopita.
 
Kiwango hicho cha mvua ni cha juu zaidi kuwahi kurekodiwa kwa zaidi ya karne moja iliyopita.
Kimbunga hicho kikali kimesababisha hali ya wasiwasi katika maeneo kadhaa Kusini mashariki mwa Uchina ambapo watu wengi wameachwa bila umeme na maji.
Katika Mkoa wa Fuji upepo mkali ulioandamana na mvua umeacha barabara kadha zimefungika na mafuriko kila mahali.
Safari za ndege na gari moshi zimesitishwa na kuwaacha mamia ya watu bila njia ya usafiri.

Karibu watu 160,000 wamehamishwa kutoka makaazi yao.
Awali kimbunga hicho kilisababisha maafa sawa na hayo katika taifa jirani la Taiwan, ambapo mamilioni ya watu hawana umeme baada ya kimbuga hicho kupiga kisiwa chote Jumamosi asubuhi.
Zaidi ya miti 2,000 iling'olewa katika kisiwa cha Taipei kutokana na kimbunga kikubwa zaidi kuwahi kutokea eneo hilo.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post