Kupitia kitengo chao cha utafiti wa kiteknolojia kampuni ya Samsung imekuja na teknolojia inayoweza kusaidia kwa kiasi kikubwa utokeaji wa ajali zinazohusisha watu kutaka kuyapita malori (ku-overtake). Ajali nyingi katika nchi zinazoendelea huwa zinatokea katika ku-overtake malori malefu bila kuona vizuri kinachokuja kwa mbele.
Teknolojia hii inahusisha utumiaji wa
kamera spesheli zilizopo mbele ya roli na kuonesha kupitia TV kubwa inayokuwa
sehemu ya nyuma ya lori. Wamedai TV hiyo iliyotengenezwa spesheli ina vioo
spesheli za kuifanya iwe salama dhidi ya uvunjikaji wa kirahisi, pia kamera
hizo zitaweza kuonesha vizuri ata wakati wa usiku.
Waandishi wengi wametoa sifa kwa
kampuni hiyo kwa wazo hili la kitofauti. Samsung wanasema teknolojia hii
itaweza kusaidia ajali za aina mbalimbali, kama vile kujua gari linalokuja
kabla ya kufanya maamuzi ya ku-overtake.. pia ajali zinazotokana na malori
kufunga breki za ghafla kutokana na wanyama au watu kuvuka barabara ghafla.