Header ads

Header ads
» » TAZAMA VIDEO: Samsung Waja na Teknolojia hii ya Kuzuia Ajali za Barabarani Zinazohusisha Malori

 

Kupitia kitengo chao cha utafiti wa kiteknolojia kampuni ya Samsung imekuja na teknolojia inayoweza kusaidia kwa kiasi kikubwa utokeaji wa ajali zinazohusisha watu kutaka kuyapita malori (ku-overtake). Ajali nyingi katika nchi zinazoendelea huwa zinatokea katika ku-overtake malori malefu bila kuona vizuri kinachokuja kwa mbele.

 amsung-safety-truck-screen-wireless-camera
Teknolojia hii inahusisha utumiaji wa kamera spesheli zilizopo mbele ya roli na kuonesha kupitia TV kubwa inayokuwa sehemu ya nyuma ya lori. Wamedai TV hiyo iliyotengenezwa spesheli ina vioo spesheli za kuifanya iwe salama dhidi ya uvunjikaji wa kirahisi, pia kamera hizo zitaweza kuonesha vizuri ata wakati wa usiku.
 

 
Waandishi wengi wametoa sifa kwa kampuni hiyo kwa wazo hili la kitofauti. Samsung wanasema teknolojia hii itaweza kusaidia ajali za aina mbalimbali, kama vile kujua gari linalokuja kabla ya kufanya maamuzi ya ku-overtake.. pia ajali zinazotokana na malori kufunga breki za ghafla kutokana na wanyama au watu kuvuka barabara ghafla.

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI


Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post