Header ads

Header ads
» » Sony yaonya watumiaji wake wa vifaa vya VAIO kutotumia mfumo mpya wa Windows 10

 Tahadhari ya kusitisha matumizi ya Windows 10

Mnamo tarehe 28 mwezi Julai, kampuni ya Microsoft ilizindua rasmi mfumo mpya wa Windows 10 kwa wapenzi wa teknolojia.
Baada ya Windows 10 kugundulika kuwa na matatizo ya uwiano katika baadhi ya vifaa, kampuni ya Sony imetoa tahadhari kwa watumiaji wa vifaa vyake vya VAIO kutotumia mfumo huo mpya.
Sony pamoja na kampuni nyingine kubwa za kutengeneza kompyuta, zinaarifiwa kuendelea kufanya majaribio ya matumizi ya Windows 10 kwenye vifaa vyao ili kuepuka matatizo ya utendajikazi wa programu.
Majaribio hayo yanatarajiwa kufanyika kwa kipindi cha mwezi mmoja au miwili, kabla ya Windows 10 kuthibitishwa kuwa na uwiano na vifaa vya kampuni mbalimbali.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post