Mfumo huo umetangazwa kuzinduliwa rasmi leo kwa ajili ya kurahisisha matumizi ya WhatsApp katika simu za iPhone.
Kutokana na maboresho hayo, watumiaji wataweza kufanya mabadiliko ya sauti za vitambulishi na mawasiliano kama wanavyopendelea.
Vile vile mfumo huo pia utawawezesha watumiaji kuhifadhi kumbukumbu za ujumbe wa maongezi yao pamoja na video za WhatsApp. Isitoshe, mfumo huo pia utakuwa na uwiano na kuhakikisha matumizi ya Apple Map iliyoboreshwa na kampuni ya Apple kwa ajili ya kutumika kwenye vifaa vyake.