Header ads

Header ads
» » Madereva watishia kufanya mugoma wa nchi nzima wiki ijayo

 Madereva wa malori wakiwa wamenyoosha mikono
Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (Tadwu) kimeazimia kufanya mgomo nchi nzima Agosti 17, mwaka huu ambao pia utahusisha daladala endapo madai yao hayatafikiwa katika kikao kitakachofanyika Alhamisi wiki hii.
Kikao hicho cha kamati maalumu iliyoundwa na Waziri Mkuu ili kujadili matatizo katika sekta ya usafirishaji, kitajadili mikataba, posho, mishahara na mazingira ya kazi kwa madereva wa Tanzania.
Akizungumza Dar es Salaam jana katika mkutano uliowakutanisha madereva 1,400, mwenyekiti wa Tadwu, Shaaban Mdemu alisema wamechoshwa na utendaji kazi wa kamati hiyo kwa sababu inapeleka ajenda nyingine bila kujadili masilahi ya madereva.
Mdemu alisema mkutano ujao utakuwa ni wa mwisho kuhudhuria na matokeo ya kikao hicho ndiyo yatakayoamua kama watafanya mgomo au la.
 Alisema madai yao yalitakiwa kumalizwa ndani ya siku saba baada ya kuundwa kwa kamati hiyo, lakini sasa ni mwezi wa tatu.
“Tunachotaka madai yetu yatekelezwe. Bila maafikiano hatutaelewana na Jumatatu ijayo hakuna dereva yeyote atakayeingiza gari barabarani,” alisema kiongozi huyo na kuungwa mkono na madereva waliohudhuria mkutano huo.
Mdemu aliwalaumu pia wamiliki wa vituo vya mafuta kwa kuwakata fedha zaidi kwa kila lita ya mafuta kwa madai kuwa wanasababisha hasara kwa kiasi kinachobainika kupungua wanapofikisha mzigo sehemu husika.
“Wamiliki wa vituo vya mafuta wanatukata Sh5,000 kwa kila lita ya mafuta yanayopungua, hili nalo tutalifikisha kwenye kamati ili lijadiliwe na kutafutiwa ufumbuzi,” alisema.
Naibu Katibu Mkuu wa Tadwu, Rashid Saleh aliwataka Watanzania wajue kuwa uamuzi wao wa kusitisha huduma unatokana na Serikali kutokuwa na dhamira ya dhati ya kutatua malalamiko ya madereva  ambayo ni ya  muda mrefu sasa.
Alisema madereva wa Tanzania hawafanani na wengine wa nchi jirani kwa sababu wana hali mbaya kimasilahi.
“Siyo lazima kila mtu anunue lori, tunataka kampuni chache zenye magari mengi na zinazolipa madereva vizuri. Hawa matajiri wenye magari mawili ndiyo wanaotusumbua kwenye masilahi,” alisema Saleh.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post