Header ads

Header ads
» » Chelsea inatarajiwa kukata rufaa dhidi ya kadi nyekundu aliyoonyeshwa Thibaut Courtois


Klabu ya Chelsea inatarajiwa kukata rufaa dhidi ya kadi nyekundu aliyoonyeshwa mlinda mlango Thibaut Courtois katika mchezo uliopigwa jumamosi dhidi ya Swansea ambao uliisha kwa droo ya magoli mawili katika uwanj wao wa nyumbani Stamford Bridge.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji huyo mwenye umri wa miaka 23 alitolewa nje dakika ya 52 baada ya kumchezea vibaya mshambuliaji Bafetimbi Gomis wa Swansea ambaye alikua anakwenda kushinda ambapo Swansea walipata penalti kutokana na faulo hiyo.
Meneja wa Chelsea Jose Mourinho alikataa kuongelea uamuzi huo baada ya kipute cha mwisho. Rufaa ya Chelsea itasikilizwa na chama cha soka nchini Uingereza FA siku ya jumanne.
Iwapo rufaa hiyo itakataliwa, Courtois ambaye anatarajiwa kufungiwa mchezo mmoja atakosekana katika safari ya kuwakabili washindi wa pili kwenye msimu uliopita Manchester City jumapili ijayo.
ikumbukwe kwamba,Asmir Begovic aliyesajiliwa kutoka klabu ya Stoke aliichezea Chelsea kwa mara ya kwanza dhidi ya Swansea baada ya kutolewa nje Courtois.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post