Leo hii Sony imetoa maelezo mtandaoni kupitia blog yake rasmi na kudhihirisha maandalizi ya muundo na muonekano mpya wa skrini za simu zake zitakazotumia Android 5.1 Lollipop.
Kulingana na picha zilizotolewa na Sony, muundo na muonekano mpya wa skrini za simu utavutia mno na kuleta msisimko kwa watumiaji.
Sony inatarajia kupokea maoni mazuri kutoka kwa wapenzi wa teknolojia baada ya kusambaza picha za muonekano huo mpya skrini za simu.