Header ads

Header ads
» » Msanii ahukumiwa kifongo cha mwaka mmoja Jela kwa kuvaa nguo fupi nchini Misri

 Mwaka mmoja jela kwa kuvaa nguo fupi Misri

Msanii mmoja ahukumiwa kifongo cha mwaka mmoja gerezani kwa kuvaa nguo isioheshimu maadili nchini Misri

Mahakama ya jijini Cairo imemuhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela muimbaji Reda al-Fouly baada ya kuonekana katika kanda yake ya video akiwa anacheza na kuimba akiwa kavalia nguo ambayo haiheshimu maadili ya Misri.
Mahakama hiyo ilifahamisha kuwa msanii huyo alikamatwa Jumapili baada ya kuonekana katika video hiyo katika mtandao wa YouTube.
Reda al-Fouly alionekana katika video hiyo akiwa kavalia nguo fupi na kuonekana mara kwa mara akiwa nusu kifua wazi akicheza.
Muandaaji wa video hiyo ambae alifahamika kwa jina la Wael Elsedeki pia alihukumiwa akiwa safarini.
Mwezi April msanii mwingine kwa jina la Safinaz alihukumiwa kifungo cha miezi 6 baada yakamatwa kavaa nguo zenye rangi ya bendera ya Misri.
Msanii huyo aliachiwa huru kwa dhamana.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post