Header ads

Header ads
» » TAARIFA: MUSWADA WA AJIRA NCHINI WAPITISHWA









Bunge la Tanzania

Bunge la Tanzania limepitisha muswada wa sheria ya udhibiti wa ajira za wageni wa mwaka 2014 ,ambapo pamoja na mambo mengine unaainisha vipengele muhimu vya ajira kwa wageni na wazawa.Hata hivyo bunge hilo limesisitiza serikali kupitia taarifa za waomba ajira wageni ili kubaini uwezo kuhusu ajira wazoomba na mienendo yao kijamii.
Sheria hiyo pia inawataka watanzania kuwepo katika ajira zote kutokana na sifa zao.huku wageni wakianishiwa aina ya ajira kulingana na mahitaji ili kuleta ushindani sahihi katika soko la ajira nchini humo.
Sheria hiyo inalenga kuvutia waombaji wenye ujuzi kutoka nje kulingana na mahitaji,huku pia ikitoa fursa kwa wazawa.Akichangia muswada huo kabla ya kupitishwa mbunge wa Karatu Yohana natse anaeleza jinsi wazawa wanavyopaswa kunufaika zaidi
Gaudensia Kabaka ni waziri wa kazi na ajira wa Tanzania na hapa amesema kuwa vibali vya kazi kwa wageni na suala la uraia kwa mjibu wa sheria hiyo ni mambo ambayo hayataenda pamoja,bali kinachotakiwa ni kutumiza masharti yote mawili.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post