Header ads

Header ads
» » TAARIFA KAMILI KUHUSU KUKAMATWA KWA GARI LA MSANII DUDE KWA TUHUMA ZA UJAMBAZI JIJI DAR


Gari la dude muda mfupi baada ya kukamatwa, Dude alitokea Polisi.
GARI la muigizaji maarufu wa filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ limekamatwa na Polisi jijini Dar es Salaam likihusishwa na tukio la ujambazi linalodaiwa kutokea Kijitonyama Mpakani usiku wa saa 5.15 Julai 21 mwaka huu.Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, gari hilo aina ya Vitz lenye namba za usajiliT 360 BAJ, lilikutwa likiwa na vijana wawili ndani yake, waliotajwa kwa majina ya Seif Jafari na Longina Ramadhani, waliotaka kupora Bajaj yenye namba za usajili T 296 CSCiliyokuwa ikiendeshwa na Seleman Khalfani.
Inadawa kuwa muda mfupi baada ya kukamatwa, Dude alitokea Polisi na kulitambua gari lake, lakini maelezo yake hayakuwatosheleza Polisi hivyo kumshikilia katika kituo kidogo cha Polisi Mabatini hadi kesho yake alipodhaminiwa.
         Muonekano wa gari hilo kwa nyuma.
Waandishi wetu walifanya jitihada za kumtafuta Dude ili azungumzie taarifa hizo, lakini aliwataka kufuatilia jambo hilo katika kituo cha Polisi, akisema suala hilo lipo mikononi mwao.
Kulwa Kikumba ‘Dude’
Shauri linalomkabili msanii huyo limefunguliwa kwa Jalada namba .KJL/RB/6399/14 UNYANG’ANYI
Credit GPL

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post