Header ads

Header ads
» » HUU HAPA UZEMBE WA CWT UNAOWAPONZA WAALIMU

 
HIZI NDIZO SABABU ZA KUTOFANIKIWA KWA MADAI YA WALIMU KUNAKOFANYWA NA CHAMA CHA WALIMU-CWT
1. POSHO KUBWA YA VIKAO. Vikao wanavyookaa serikali na CWT upo ushahidi kwamba serikali inatoa kiasi kikubwakama posho za vikao pindi wanapokutana na viongozi wa juu wa CWT. Kwa kikao kimoja posho si chini ya million 1.5 . hivyo viongozi wa CWT hawako tayari kumaliza makubaliano ili waendelee kula posho. Mfano makubaliano ambayo serikali ilitoa kwa CWT ni nyongeza ya 24% na badala yake wameongeza kwa wastani wa 8%.
2. VIONGOZI WA CWT HAWAWAKILISHI WALIMU AMBAO NI WANACHAMA WAO, kwa sababu zifuatazo;-
i. Viongozi ni matajiri mno hivyo unapozungumzia ugumu wa maisha kwa walimu wao hawayaoni. Mfano Raisi wa CWT Ndugu Mkoba anamiliki na anaishi kwenye nyumba ya kibepari ya ghorofa mbili. Je, ni kweli atamkumbuka mwl wa hali ya chini ambaye amepanga chumba na sebule kijijini??
ii. Hela za chama-CWT hazina kazi ya kufanya nje ya kulipa mishahara  na posho mbalimbali kama vile safari, vikao n.k
3. Kuanzisha migomo kwa kukurupuka. Ikumbukwe mgomo wa Walimu wa August mwaka jana 2012, ulikuja tu baada ya Vuguvugu la kuanzisha mbadala wa CWT uitwao Umoja wa Maafisa Elimu Tanzania (UMET). Hivyo CWT iliamua kuitisha mgomo ili kuwalidhisha  wanachama wake wasihame na kuunga mkono UMET, kukurupuka huko kwa CWT ndiko kuliko sababisha CWT Kutofanikisha mgomo wake.
4. KUKAA KIMYA KWA WALIMU. Walimu tumekaa kimya sana hatuhoji utendaji kazi wa CWT ndiyo maana hawaoni haja ya kuwajibika kwa wanachama wao, hii hutulazimu sisi wanachama tufatilie madai mbalimbali bila msaada wa chama mfano kupanda daraja, nauli za likizo, malimbikizo ya mshahara n.k
5. VIONGOZI WA CHAMA KUWA NA POSHO AU MISHAHARA NJE YA AJIRA YA SERIKALI. Viongozi wa CWT wanauhakika kwani wanavipato zaidi ya kimoja tofauti na walimu ambao wanategemea mshahara tu.

MAPENDEKEZO.
1. Walimu tuwe wakali kwa viongozi wa CWT ili kuwafanya wawajibike mfano CWT haitoi elimu kwa wanachama juu ya haki na wajibu wa wanachama, hata katiba ya CWT wanachama hawana.
2. CWT itoe fedha kwa walimu na wanachama ambao wamemaliza muda wa utumishi kama kustaafu au kufariki. Hii itasaidia kutumika kwa fedha ambazo walimu wanachangia kwa muda wote wakiwa watumishi na baada ya ukomo wa utumishi hawanufaikii na chochote. 
3. CWT ipunguze asilimia ya kukata wanachama wake kutoka 2% ya sasa hadi 0.5% ili kuepuka kuwa nafedha nyingi ambazo haziwanufaishi wanachama. Pendekezo la punguzo la tozo hii linafuatia CWT kuwa na vitega uchumi kama vyanzo vingine vya mapato.
4. Walimu tuwe na umoja na ushirikiano na tushinikize chama kuitisha mgomo mapema iwezekanavyo ili kupinga  ongezeko la wastani wa 8% na hivyo tupate nyongeza zaidi ya 150% ili kuweka usawa wa kisekta kati ya kada ya afya, kilimo na ualimu, ambazo kada hizo wamewazidi walimu mshahara mkubwa mno Hii ni kwa mujibu wa waraka wa watumishi wa serikali Na 1.  Wa mwaka 2013, wenye Kumb. Na. CAC.205/228/01/C/14 wa Julai 2, 2013 uliosainiwa na Katibu mkuu Utumishi Ndugu George D.
NGAZI YA ELIMU UALIMU/ ELIMU KILIMO AFYA
Certificate (Cheti) Tsh 344,000/= Tsh 1,060,000/= Tsh 562,000/=
Diploma (Stashahada) Tsh 432,500/= Tsh 1,252,000/= Tsh 821,000/=
Degree (Shahada) Tsh 589,000/= Tsh 1,473,000/= Tsh 994,000/=HIZI NDIZO SABABU ZA KUTOFANIKIWA KWA MADAI YA WALIMU KUNAKOFANYWA NA CHAMA CHA WALIMU-CWT
1. POSHO KUBWA YA VIKAO. Vikao wanavyookaa serikali na CWT upo ushahi
di kwamba serikali inatoa kiasi kikubwakama posho za vikao pindi wanapokutana na viongozi wa juu wa CWT. Kwa kikao kimoja posho si chini ya million 1.5 . hivyo viongozi wa CWT hawako tayari kumaliza makubaliano ili waendelee kula posho. Mfano makubaliano ambayo serikali ilitoa kwa CWT ni nyongeza ya 24% na badala yake wameongeza kwa wastani wa 8%.
2. VIONGOZI WA CWT HAWAWAKILISHI WALIMU AMBAO NI WANACHAMA WAO, kwa sababu zifuatazo;-
i. Viongozi ni matajiri mno hivyo unapozungumzia ugumu wa maisha kwa walimu wao hawayaoni. Mfano Raisi wa CWT Ndugu Mkoba anamiliki na anaishi kwenye nyumba ya kibepari ya ghorofa mbili. Je, ni kweli atamkumbuka mwl wa hali ya chini ambaye amepanga chumba na sebule kijijini??
ii. Hela za chama-CWT hazina kazi ya kufanya nje ya kulipa mishahara na posho mbalimbali kama vile safari, vikao n.k
3. Kuanzisha migomo kwa kukurupuka. Ikumbukwe mgomo wa Walimu wa August mwaka jana 2012, ulikuja tu baada ya Vuguvugu la kuanzisha mbadala wa CWT uitwao Umoja wa Maafisa Elimu Tanzania (UMET). Hivyo CWT iliamua kuitisha mgomo ili kuwalidhisha wanachama wake wasihame na kuunga mkono UMET, kukurupuka huko kwa CWT ndiko kuliko sababisha CWT Kutofanikisha mgomo wake.
4. KUKAA KIMYA KWA WALIMU. Walimu tumekaa kimya sana hatuhoji utendaji kazi wa CWT ndiyo maana hawaoni haja ya kuwajibika kwa wanachama wao, hii hutulazimu sisi wanachama tufatilie madai mbalimbali bila msaada wa chama mfano kupanda daraja, nauli za likizo, malimbikizo ya mshahara n.k
5. VIONGOZI WA CHAMA KUWA NA POSHO AU MISHAHARA NJE YA AJIRA YA SERIKALI. Viongozi wa CWT wanauhakika kwani wanavipato zaidi ya kimoja tofauti na walimu ambao wanategemea mshahara tu.

MAPENDEKEZO.
1. Walimu tuwe wakali kwa viongozi wa CWT ili kuwafanya wawajibike mfano CWT haitoi elimu kwa wanachama juu ya haki na wajibu wa wanachama, hata katiba ya CWT wanachama hawana.
2. CWT itoe fedha kwa walimu na wanachama ambao wamemaliza muda wa utumishi kama kustaafu au kufariki. Hii itasaidia kutumika kwa fedha ambazo walimu wanachangia kwa muda wote wakiwa watumishi na baada ya ukomo wa utumishi hawanufaikii na chochote.
3. CWT ipunguze asilimia ya kukata wanachama wake kutoka 2% ya sasa hadi 0.5% ili kuepuka kuwa nafedha nyingi ambazo haziwanufaishi wanachama. Pendekezo la punguzo la tozo hii linafuatia CWT kuwa na vitega uchumi kama vyanzo vingine vya mapato.
4. Walimu tuwe na umoja na ushirikiano na tushinikize chama kuitisha mgomo mapema iwezekanavyo ili kupinga ongezeko la wastani wa 8% na hivyo tupate nyongeza zaidi ya 150% ili kuweka usawa wa kisekta kati ya kada ya afya, kilimo na ualimu, ambazo kada hizo wamewazidi walimu mshahara mkubwa mno Hii ni kwa mujibu wa waraka wa watumishi wa serikali Na 1. Wa mwaka 2013, wenye Kumb. Na. CAC.205/228/01/C/14 wa Julai 2, 2013 uliosainiwa na Katibu mkuu Utumishi Ndugu George D.
NGAZI YA ELIMU UALIMU/ ELIMU KILIMO AFYA
Certificate (Cheti) Tsh 344,000/= Tsh 1,060,000/= Tsh 562,000/=
Diploma (Stashahada) Tsh 432,500/= Tsh 1,252,000/= Tsh 821,000/=
Degree (Shahada) Tsh 589,000/= Tsh 1,473,000/= Tsh 994,000/=
CREDIT: MWANA CCM DAMU - FACEBOOK
BAHTISMA BLOG CHAGUO LA WATU

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post