Header ads

Header ads
» » Serena Williams azidi kutamba kwenye tenisi, ashinda Grand Slam yake ya 20

Serena Williams anyakuwa taji la Roland Garros

Mashindano ya Roland Garros French Open yalifika kileleni hapo jana ambapo mwanatenisi wa Marekani Serena Williams na Lucie Safarova kutoa Czech walitoana jesho katika mechi ya fainali.
Mkali wa tenisi Serena Williams alimshinda Lucie Safarova seti 2 – 1 za msururu wa 6-3, 6-7 na 6-2, na kushinda taji la Roland Garros kwa mara ya tatu.
Wakati huo huo, Serena Williams ameweza kufikisha Grand Slam 20 katika mkusanyiko wake wa mataji makuu ya mashindano ya tenisi.
Serena Williams mwenye umri wa miaka 33 sasa ameweza kupiga hatua zaidi na kukaribia rekodi ya ushindi wa Grand Slam 22 inayoshikiliwa na mwanatenisi wa zamani wa Ujerumani Steffi Graf.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post