Header ads

Header ads

headlines

    3:02 PM
» » POLISI WAZIDIWA NGUVU NA RAIA WENYE ASIRA KALI!!!,WAPOKONYWA WAHARIFU NA KUWACHOMA MOTO

Hii si poa! Raia wenye hasira, katikati ya wiki iliyopita waliwachukua vijana wawili wanaotuhumiwa kuwa majambazi, waliokuwa mikononi mwa polisi, ambao majina yao yametajwa kuwa ni Mnubi na White kisha kuwateketeza kwa moto baada ya kuwabaini kuwa ndiyo waliohusika na uvamizi na uporaji wa maduka mawili ya huko Mwika-Madukani, Moshi vijijini.
Chanzo chetu kililiambia gazeti hili kuwa, vijana hao wakiwa na silaha, walionekana wamepanda pikipiki moja na kuvamia maduka hayo mawili na kupora fedha kiasi ambacho bado hakijajulikana, kabla ya kutoweka.

Kesho yake walikamatwa na wananchi walioshirikiana na polisi, baadaye kukatokea kutoelewana baada ya jeshi hilo kutaka kuwachukua ili kuwapeleka mbele ya sheria.

“Polisi waliwaweka katika gari lao ili waondoke nao, lakini wananchi waliwachomoa na kuwapa kipigo kisha kuwateketeza kwa moto, askari walijaribu hata mabomu ya kutoa machozi, lakini wakazidiwa,” kilisema chanzo hicho.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Godfrey Kamweli alikiri kutokea kwa tukio hilo.

Imehaririwa na;- Unknown

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Mbio za Urais CCM: Benard Membe Ataka Jina la Edward Lowassa Lisikatwe.......Atamani Akutane Naye Tatu Bora Ili Amwonyeshe Uwezo Wake
»
Previous
Dunia na Visa: Kutana na Bibi mwenye umri wa miaka 65,aliyepata mimba ya pacha wanne