Header ads

Header ads
» » » Yamoto Band kutoa burudani katika mchezo wa Yanga na SC Villa


Kundi la Yamoto Band
Bendi ya muziki wa bongo fleva Yamoto, inatarajia kutoa burudani katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki kati ya Yanga na Sports Villa ya Uganda, mchezo utakaofanyika Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Nyumbani Kwanza, Mossy Magere, alisema kuwa katika mchezo huo kutakua na burudani mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoka kwa Yamoto Band.
Alisema kuwa wasanii hao wanatarajiwa kutoa burudani ya aina yake kwa mashabiki wa mpira watakaojitokeza kwa ajili ya kuchangia fedha za kujenga kituo cha watu wanaoishi katika mazingira magumu ikiwa ni pamoja na walemavu wa ngozi (albino).
“Bendi ya Yamoto ndio inatarajia kutoa burudani ya aina yake katika mchezo huo wa kirafiki wa Kimataifa ambao utatanguliwa na mchezo wa mashabiki wa Yanga dhidi ya Manchester United,” alisema.

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post