Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetoa msaada wa mabati 850 ikiwa ni ahadi iliyotolewa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kusaidia waathirika wa mafuriko katika kijiji cha Mwakata wilayani Kahama.Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa (pichani), alisema msaada huo una thamani ya Sh. milioni 12.Dk. Slaa alifafanua kuwa kati ya kiasi hicho cha fedha zilizonunua mabati, Sh. milioni 10 ni sehemu ya ruzuku inayotolewa na serikali kwa chama hicho na kiasi kingine ni michango iliyopatikana katika mikutano ya hadhara ya chama hicho iliyofanyika mjini Kahama.Alisema waliamua kununua mabati hayo kutokana na kamati ya mkoa inayoratibu maafa hayo ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga, kupendekeza vinunuliwe vifaa vya ujenzi kutokana na chakula kuwapo cha kutosha.
Dk. Slaa aliwataka viongozi kuhakikisha wanasimamia vema ujenzi wa nyumba za kuduma za makazi ya wananchi wa kata ya Mwakata kama ilivyopendekezwa na Rais Jakaya Kikwete, alipotembelea waathirika hao kwani mara nyingi serikali imekuwa ikishindwa kutekeleza kwa wakati majanga kama hayo.“Niwaombe viongozi wa mkoa kusimamia waathirika hawa wajengewe nyumba kwamuda mwafaka…
Watanzania wengi tanawakatisha tamaa kutokana na kushindwa kutimiza ahadi zinazotolewa kama kule Kilosa hadi leo bado watu wanaishi kwenye mahema, tangu nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, naomba sana Shinyanga muwe wamfano,” alisema Dk. Slaa.
Katika hatua nyingine, misaada imeendelea kutolewa kwa waathirika hao baada ya Kampuni ya Simu (TTCL), kutoa chakula na vitu mbalimbali vyenye thamani ya Sh. milioni tatu.Meneja wa TTCL Mkoa wa Shinyanga, Peter Kuguru, alisema kampuni yake imeungana na Watanzania wengine walioguswa na maafa hayo kutoa msaadawa kibinadamu na kuyaasa mashirika mengine na watu mbalimbali kujitokeza kuwasaidia wananchi hao.
Topics: MATUKIO
Imehaririwa na;- Unknown
Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.

Playstore
TeknoTaarifa Video
TAARIFA ZILIZOSOMWA SANA
-
Mambo vipi Rafiki yangu? Kama wewe ni miongoni mwa watu wanaopendelea kuweka Pattern kwenye simu zenu kwa usalama zaidi, Basi msijali...
-
Hivi karibuni mdau mmoja wa Website hii alinitumia e-mail na kuniuliza ni kwa jinsi gani anaweza kuipata simu yake iliyo...
-
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Habari Ikulu,Salva Rweyemamu amenukuliwa na Redio BBC Swahili akisema kuwa Rais wa Burundi,Pierre Nkurunziza ha...
-
Kampuni moja ya Florida, Marekani imekuja na dhana ya kujenga meli ‘Freedom Ship’, itakayokuwa na uwezo wa kuwa na kila kitu ch...
-
Si wengi wetu wanaofahamu umuhimu wa kula samaki mara kwa mara na jinsi kitoweo hiki kilivyo na umuhimu wa kipekee katika afya ya bina...
-
Kwa kawaida wajasiriamali wengi hasa wadogo wadogo huzingatia mipango ya kukuza mitaji, kuimarisha uwezo wa wafanyakazi, kukuza faida, k...
-
Mwana wa Sokwe anaendelea vyema baada ya kuzaliwa kupitia upasuaji katika hali isiyo ya kawaida. Sokwe huyo anayetoka upande wa magha...
-
Kama ni mpenzi wa vitu vikali na bora na umejipanga kuchukua Mzigo mpya wa Kompyuta mpakato “Laptopo” kwa Mwaka huu 2016,Ni...
-
Mkurugenzi mkuu wa Facebook Mark Zuckerberg amenunua nyumba 4 kwa ajili ya kuzibomoa na kujenga upya katika eneo la Palo Alto lililok...
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini, TCRA imetoa tamko kuhusiana na malalamiko kutoka kwa watumiaji wa huduma za simu nchini kufuatia kuba...
Data Boosta
