Header ads

Header ads
» » » Mfumo wa Simu za Apple wagundulika kuvujisha Taarifa xa Watumiaji


Uvumbuzi huo ulifanyika baada ya wakili anayetetea haki za kibinadamu kutoa taarifa kwa watafiti wa masuala ya usalama kuhusu jumbe alizozipata bila kutarajia.
Waligundua taarifa nyingine tatu za awali zisizofahamika zilizovuja kutoka kwa mfumo wa Apple .
tangu wakati huo Apple imetoa taarifa ya kuelezea tatizo hilo na namna linavyoshughulikiwa na kampuni hiyo.
Makampuni mawili ya usalama yaliyohusika , Citizen Lab na Lookout, yamesema yamehifadhi taarifa hizo za uvumbuzi hadi suala hilo litakapopatiwa ufumbuzi.

 mwanaharakati wa haki za binadamu Ahmed Mansoor

Kampuni ya Citizen Lab inasema , simu yake ya iPhone 6 ingekuwa ''imefunguliwa'' , ikimaanisha mfumo mwingine ambao haukuidhinishwa ungelikuwa umewekwa kwenye simu yake.
"Na kama simu yake ingeathiriwa , ingekuwa kifaa cha upelelezi cha digitali ndani ya mfuko wake wa nguo, yenye uwezo wa kung'amua taarifa kwa kutumia kamera na kipaza sauti cha simu kurekodi simu zake za WhatsApp na Viber , kuingia kwenye jumbe alizotuma kwa simu na kuweza kumfuatilia kote anakoenda," ilisema kampuni ya Citizen Lab.
"Hatuna taarifa zozote za matukio ya aina hii ya iPhone suala linalofanya tukio hili kuwa la nadra ."
Watafiti wanasema wanaamini mfumo huu wa uchunguzi unaohusisha spyware ulibuniwa na kampuni ya NSO Group, ya Israel ya ''vita vya mitandaoni"

Imehaririwa na;- poatel Africa

Habari yako! Endelea kutembelea Tovuti ya TeknoTaarifa kwa Taarifa murwa za Teknolojia kutoka ndani na nje ya Tanzania, Tupo kwa ajili ya wapenzi wa Teknolojia.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post